Synopsis
Makala ya Wimbi la Siasa inakupa fursa ya kufahamu masuala ya kisiasa yanayoendelea ndani na nje ya Bara la Afrika. Kwenye Makala haya utapata habari ambazo zinakugusa moja kwa moja wewe msikilizaji. Kila wakati usikose kusikiliza Makala ya Wimbi la Siasa
Episodes
-
Uchaguzi mkuu wa Ghana: Chama tawala NPP kushindwa na chama cha upinzani NDC unatoa funzo gani?
12/12/2024 Duration: 10minNchini Ghana, rais wa zamani John Dramani Mahama alipata ushindi mkubwa na kumaliza uongozi wa miaka minane wa chama tawala New Patriotic Party (NPP) chake rais Nana Akufo-Addo, anayeondoka madarakani baada ya kuongoza kwa mihula miwili.
-
Umoja wa Mataifa unaadhimisha Siku 16 za Unaharakati dhidi ya Dhuluma za Kijinsia
30/11/2024 Duration: 10minSiku 16 za uanaharakati dhidi ya ukatili wa kijinsia ni kampeni inayofanyika kila mwaka kati ya Novemba 25 hadi Desemba 10. Ni kampeni ya siku 16 inayolenga kuhamasisha umma jinsi ya kukomesha ukatili dhidi ya wanawake na wasichana. Siku hiyo ilianza kuadhimishwa rasmi mwaka 1991,siku hii inaongozwa na Kituo cha kimataifa cha Wanawake tarehe 10 ilichaguliwa rasmi kuwa siku ya kilele cha maadhimisho haya ikiambatana na siku ya haki za binadamu duniani. Asante kwa kuendelea kuwa muaminifu kwa radio yako na kwa mtangazaji wako unaweza kumfollow kwa kubonyeza hapa Billy Bilali
-
Wakaazi wa jimbo la Somaliland wapiga kura kumchagua rais na wabunge
13/11/2024 Duration: 10minWakaazi wa jimbo la Somaliland, mojawapo wa êneo lililojitenga na Somalia zaidi ya miaka 30 iliyopita, tangu mwaka 2003 wamekuwa wakishiriki kwenye uchaguzi wa kumchagua rais na wabunge wao. Fursa hiyo pia imekuja Novemba tarehe 13 mwaka 2024 ambapo wapiga kura Milioni 1 waliondikishwa na Tume ya Uchaguzi ya Somaliland wanamchagua rais atakayewatumikia kwa miaka metano.Wagombea watatu wanatafuta urais wa jimbo hilo, akiwemo kiongozi wa sasa Muse Bihi Abdi, anayetaka muhula wa pili, lakini mpinzani wake mkuu ni Abdirahman Mohamed Abdullahi, maarufu kwa jina la "Irro,”.Kwenye Makala ya Wimbi la Siasa, tunajadili umuhimu wa uchaguzi wa jimbo la Somaliland na umuhimu wake, kwenye Jumuiya ya Kimataifa, wakati huu, êneo hilo linapotaka kujitawala.
-
Msumbuji : Upinzani wakataa kutambua ushindi wa Daniel Chapo
05/11/2024 Duration: 10minNchini Musumbuji maandamano yamekuwa yakishuhudiwa baada ya upinzani kukataa kutambua ushindi wa mgombea wa chama tawala Daniel Chapo. Aliyekuwa mgombea wa upinzani Venancio Mondlane, amekuwa akisisitiza kwamba alipokonywa ushindi, katika makala haya tunazama kujadili kile kinachoendelea nchini Musumbiji.Wachambuzi wa siasa za kimataifa Lugete Mussa Lugete na Felix Arego wanafafanua hali nchini Msumbiji.