Synopsis
Fahamu masuala kadha wa kadha kuhusu uchumi kama vile, namna ya kupambana na umaskini, mfumuko wa bei, kushamiri kwa matumizi ya dola na athari za kuyumba kwa uchumi wa dunia kwa nchi za Afrika. Mada hizi zinafanyiwa utafiti wa kina na zinazungumzwa kwa lugha rahisi inayoeleweka ili kukufanya uelewe na usichoke kusikiliza .
Episodes
-
Manufaa na changamoto za mkataba wa biashara huria barani Afrika, AfCFTA
04/12/2024 Duration: 10minMsikiliza mataifa 54 ya Afrika yametia saini mkataba wa biashara huria barani Afrika, mataifa 48 yakitia saini itifaki kuanza kuutekeleza. Huu ni moja ya mikataba mikubwa ya kibiashara duniani, ukitarajiwa kuwaondoa raia milioni 30 kutoka kwenye umasikini na kuongeza mapato ya bara hil hadi kufikia dola bilioni 450 ifikapo mwaka 2030.Kuangazia kwa kina mkataba huu pamoja na hali ya madeni ya nchi za Afrika, tumezungumza na Ali Mkimo, mtaalamu na mchambuzi wa masuala ya uchumi akiwa Tanzania.
-
Vijana pwani ya Kenya waachana na dawa za kulevya na kugeukia shughuli za kiuchumi
13/11/2024 Duration: 10minMsikilizaji kwa muda sasa, eneo la pwani ya Kenya limekuwa likikabiliwa na kiwango kikubwa cha matumizi ya dawa za kulevya miongoni mwa vijana, Hali hii ikichangia vitendo vya utovu wa nidhamu, kuongezeka kwa magonjwa ya zinaa na ndoa za mapema. Hata hivyo, kutokana na juhudi za mashirika mbalimbali ya kijamii na yasiyo ya kiserikali, vijana wengi walioacha kutumia dawa za kulevya sasa wanajihusisha na miradi ya kibiashara ili kujikimu.Makala ua Gurudumu la Uchumi juma hili, inawaangazia vijana wa eneo la Pwani ambao wameamua kuachana na matumizi ya dawa za kulevya.
-
Sehemu ya pili: Je kuongeza kodi ni suluhu kwa matatizo ya Afrika
07/11/2024 Duration: 10minMsikilizaji kwa muda sasa mataifa ya Afrika yameendelea kupitia changamoto za kifedha, kuanzia katika kukusanya mapato na matumizi kwa ajili ya maendeleo yake, hali ambayo imesababisha nchi nyingi kujikuta pabaya kutokana na kulazimika kukopa fedha toka kwa taasisi za kimataifa au nchi zilizoendelea huku ziklipa riba kubwa katika urejeshaji.Lakini je, kuongza kodi ndio suluhu? Mchambuzi wa masuala ya uchumi kutoka Tanzania, Ali Mkimo anafafanua.
-
Je, nyongeza ya kodi ni suluhu kwa nchi zinazoendelea kujikwamua kiuchumi
30/10/2024 Duration: 10minMataifa ya Afrika yameendelea kupitia changamoto za kifedha, katika kukusanya mapato kwa ajili ya maendeleo, hali ambayo imesababisha nchi nyingi kujikuta pabaya kutokana na kulazimika kukopa fedha toka kwa taasisi za kimataifa au nchi zilizoendelea huku ziklipa riba kubwa katika ureje shaji.Lakini je, kuongeza wigo wa kodi kwa mataifa yanayoendelea ndio njia pekee kuwezesha mataifa haya kujikwamua kiuchumi? Tumezungumza na Ali Mkimo, mchambuzi na mtaalamu wa masuala ya uchumi akiwa Tananzania