Habari Rfi-ki

  • Author: Vários
  • Narrator: Vários
  • Publisher: Podcast
  • Duration: 3:37:54
  • More information

Informações:

Synopsis

Makala ya kila siku yanayompa fursa msikilizaji kutoa maoni yake juu ya habari zilizopewa uzito wa juu kwa siku husika. Msikilizaji hushiriki kwa kutuma ujumbe mfupi pamoja na kupiga simu.

Episodes

  • Kauli ya rais wa Tanzania Samia Suluhu kuwazuia wanaharakati wa nchi zingine

    20/05/2025 Duration: 09min

    Leo tunaangazia ,hatua ya  Tanzania kuwazuia  Mawakili, wanaharakati wa haki za binadamu kutoka nchini Kenya, akiwemo Jaji Mkuu mstaafu Willy Mutunga  waliokwenda kusikiliza kesi ya uhaini inayomkabili kiongozi mkuu wa upinzani Tundu Lissu. Rais Samia Suluhu Hassan, amesema serikali yake haitaruhusu wanaharakati wa kigeni kuingia nchini Tanzania na kuingilia masuala ya ndani ya nchi yake.

  • Nini kifanyike kumaliza vita vinavyoendelea Sudan,Ukraine na Gaza

    19/05/2025 Duration: 10min

    Viongozi wa dunia, wameendelea kutoa wito wa amani kwenye nchi  za Sudan Ukraine na Gaza hizo, ambako vita vimesababisha vifo vya maelfu ya raia na wengine kuwa wakimbizi. Hata hivyo licha ya wito huu, mapigano yameendelea kuripotiwa.

  • Hali ya mafuriko katika mataifa ya Afrika Mashariki na pembeya Afrika

    13/05/2025 Duration: 09min
  • Maoni ya waskilizaji kuhusu vipindi vyetu juma hili

    09/05/2025 Duration: 09min

    Juma hili waskilizaji wetu walikuwa na maoni haya kuhusu taarifa zetu

  • Je kuna hofu ya kutokea kwa vita vya tatu vya dunia

    08/05/2025 Duration: 10min

    Katika makala haya  tunajadili athari ya vita vya ukraine na Urusi na sasa tishio la vita nyingine kati ya India na Pakistan. Je ni shara ya kutokea kwa vita vya pili vya dunia ? ndilo swali tumekuuliza. Skiza baadhi ya maoni ya waskilizaji.

  • News Zealand kudhibiti mitandao ya kijamii kwa watoto

    07/05/2025 Duration: 09min

     Shaba ya makala haya inalenga news Zealand ambapo serikali inapendekeza marufuku ya matumizi ya mitandao kwa watoto walio na umri wa chini ya miaka 16, lengo likiwa kuwakinga dhidi ya athari za mitandao. Njia gani wazazi wa kiafrika wanaweza kuwalinda watoto na mitandao ya kijamii? Ndilo swali tumeuuliza na haya hapa baadhi ya maoni yako, skiza makala haya.

  • Dunia uhuru wa vyombo vya habari na wanahabari

    05/05/2025 Duration: 09min

    Leo mada yetu inajikita kwa siku ya kimataifa ya uhuru wa vyombo vya habari, ambapo  Umoja wa Mataifa umesema licha ya baadhi ya nchi kupiga hatua katika ulinzi wa wanahabari, hofu ya uhuru wa habari kuendelea kuminywa inaendelea kutanda. Mwaka jana jumla ya wanahabari 82 walipoteza maisha wakitekeleza majukumu yao. Tuambie nchini mwako vyombo vya habari viko huru? Haya hapa baadhi ya maoni yako, skiza makala.

  • Makala habari rafiki Ijumaa Mada huru

    02/05/2025 Duration: 09min
  • Rasimu ya makubaliano kati ya DRC na Rwanda ya kutafuta suluhu ya mzozo

    29/04/2025 Duration: 09min
  • Mchakato wa kumchagua kiongozi mpya wa kanisa katoliki duniani

    28/04/2025 Duration: 10min

    Kwa sasa macho yakiwamulika makadinali 135 watakaochagua papa mpya ndani ya siku chache zijazo, mjadala kuhusu Papa kutoka Afrika ukishamiri.Mchakato wa kumchagua p

  • Joseph Kabila adaiwa kurejea DRC kupitia Goma

    21/04/2025 Duration: 09min

    Juma lililopita ripoti ambazo hazijathibitishwa rasmi zilieleza kuwa rais wa zamani wa DRC, Joseph Kabila alirejea nchini Mwake kupitia mji wa Goma unaokaliwa na waasi wa M23 wanaosaidiwa na Rwanda. Hata hivyo hatua yake imeifanya serikali ya Kinshasa, kusimamisha shughuli zote za chama chake cha PPRD, ikikituhumu kushurikiana na waasi hao.Unazungumziaje kurejea kwa rais Kabila?Ndilo swali tumekuuliza katika makala haya.Skiza maoni ya mskilizaji.

  • DRC: Kujerea kwa Joseph Kabila kwaibua hisia mseto

    10/04/2025 Duration: 10min

    Katika makala haya shaba yetu inalenga nchini DRC, ambapo Rais mustaafu wa DRC, Joseph Kabila, ametangaza kurejea nchini humo, kutoka nchini Afrika Kusini ambako amekuwa akiishi kwa zaidi ya mwaka moja , ili kuchangia kutafuta suluhu kwa mzozo wa usalama mashariki mwa nchi yake. Unazungumziaje hatua hii ya Kabila? Ndilo swali tulikuuliza, skiza makala haya kuskia maoni ya waskilizaji wetu.

  • Marekani : Rais Donamd Trump atangaza ushuru zaidi kwa bidhaa za kigeni

    09/04/2025 Duration: 10min

    Kwenye makala haya tunajadili,  hatua ya rais wa Marekani, Donald Trump kutangaza kuongeza ushuru kwa bidhaa zote zanazoingizwa Marekani, kutoka mataifa ya Kigeni, hatua inayoonekana kutikisa uchumi wa Dunia.  Je unahisi hatua ya rais Trump ni sahihi?Ndilo swali tumeuuliza.Skiza makala haya kujua maoni ya waskilizaji.

  • Kenya: Yawarejesha nyumbani raia wake waliotapeliwa kuenda Mynamar

    08/04/2025 Duration: 09min

    Shaba yetu kwenye makala haya inalenga hatua ya Serikali ya Kenya, kueeendelea kuwarejesha mamia ya raia wake waliotapeliwa na kusafirishwa hadi nchini Myanmar kwa ahadi ya kupewa ajira.  Nchini mwako visa kama hivi vinaripotiwa?Ndilo swali letu, skiza makala haya kuskia baadhi ya maoni ya waskilizaji.

  • Africa Mashariki : Viongozi watathimini kudhibiti mitandao ya kijamii

    08/04/2025 Duration: 09min

    Katika makala haya tunajadili haja ya kuwepo sheria za kudhibiti mitandao ya kijamii kwa baadhi ya mataifa ya Africa Mashariki. Skiza makala haya kuskia mano ya waskilizaji wetu.

  • Maoni ya waskilizaji kuhusu wizi unaofanywa kwenye mizani na wafanyabiashara

    05/04/2025 Duration: 10min

    Makala haya ni maoni ya waskilizaji kuhusu ripoti maalum ya namna wananchi wanavyopigwa na wafanyabiashara kwenye mizani wanapopimiwa nafaka mbalimbali za chakula, huku gesi ya kupikia pia ikitajwa.

  • Maoni yako kwenye makala ya Habari Rafiki Mada Huru Ijumaa

    28/03/2025 Duration: 10min
  • DRC: Majadiliano ya kitaifa kuhusu kuundwa kwa Serikali ya Umoja wa kitaifa

    25/03/2025 Duration: 10min
  • Qatar : Yakutanisha Kagame na Tshisekedi

    20/03/2025 Duration: 09min

    Shaba yetu  leo kwenye makala haya inalenga taifa la Qatar ambapo taifa hilo juma hili lilifanikiwa kuwaleta pamoja marais Felix Tshiesekedi wa DRC na mwenzake wa Rwanda Paul Kagme, katika juhudi za kutafuta suluhu kwa mzozo wa mashariki ya DRC. Unafikiri Qatar itafanikiwa kuzima mzozo wa mashariki mwa DRC. Skiza makala haya kujua baadhi ya maoni ya waskilizaji.

  • Kenya : Kanisa katoliki latangaza marufuku kwa wanasiasa

    19/03/2025 Duration: 10min

    Tunajadili  hatua ya Kanisa la Anglikana nchini Kenya, kwa mara nyingine limesisitiza marufuku ya kuwazuia wanasiasa kuzungumza kanisani katika juhudi za kuzuia wanasiasa kufanya siasa kanisani. Je unazungumziaje hatua hii ya kanisa Anglikana nchini Kenya? Skiza makala haya kuskia baadhi ya maoni ya waskilizaji wetu.

page 1 from 2